BREAKING NEWS


AJALI YA JAHAZI MV MUNA

Watu 12 wamenusurika kufa baada ya jahazi la mizigo liitwalo MV Muna lenye namba za usajili T.0083 liliyokuwa na mizigo kiasi cha tani 50 likitokea  nchini Kenya kwenda Visiwani Zanzibar kuzama katika eneo la Kigombe  Wilayani Muheza usiku wa kuamkia leo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constatine Massawe amethibitisha kutokea tukio hilo na kueleza kuwa kuzama kwa jahazi kulitokana na mashine zake kugoma na kuanza kuzama.

Abiria waliosalimika wamepelekwa hospitali ya rufaa ya Bombo Mkoani Tanga kwa ajili ya kuchunguzwa afya zao kutokana na dhoruba walikuwa wameipata wakati Jahazi hilo lilipokuwa limezama.


Written by

0 comments: