Mkuu Wa Mkoa Wa Tanga Azindua Mpango Mkakati Wa Miaka Mitano Wa Ukimwi Katika Mkoa Wa Tanga Wakati Wa Kikao Cha RCC


Mhe. Magalula Said Magalula , Mkuu wa Mkoa wa Tanga akikata utepe uliofungwa kwenye kitabu kuashiria  uzinduzi wa Mpango wa Miaka mitano wa Ukimwi katika Mkoa wa Tanga wakati wa kikao cha Ushauri cha Mkoa wa Tanga (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga mwishoni mwa wiki.

Mada mbalimbali ziliwasilishwa na kujadiliwa katika kikao hicho zikiwemo mada juu ya Taarifa ya upatikananji maji katika Mkoa wa Tanga, taarifa ya Bima ya Afya, taarifa ya hali ya bandari ya Tanga, taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya 2014/2015 na mapenekezo ya bajeti ya mwaka 2015/2016.

Wajumbe walipata nafasi ya kujadiliana jinsi ya kuboresha huduma na vilevile mikakati juu ya kukabiliana na baadhi ya changamoto. Naye Mkuu wa mkoa ambaye alikuwa Mwenyekiti wa kikao alitoa maelekezo juu ya nini kifanyike ili huduma za wananchi ziweze kuboreshwa. 

    Baadhi ya Wajumbe na waalikwa wakisikiliza mijadala mbalimbali



      Baadhi ya waandishi wa habari wakisikiliza kwa makini



Written by

0 comments: