Mbuga ya Saadani, Hifadhi yenye vitu ambavyo havipatikani katika Mbuga nyingine


Japo si maarufu miongoni mwa wengi lakini Saadani ni hifadhi ya kipekee yenye vivutio vizuri vya kitalii vinavyoweza kulitangaza taifa na kuongeza pato lake.
Mbuga ya Saadani ni miongoni mwa hifadhi 16 za taifa. Hifadhi hii iko chini ya Mamlaka za Hifadhi za Taifa (Tanapa) ilianzishwa mwaka 1962 ikiwa ni pori la akiba. Baadaye mwaka 2005, ilipandishwa hadhi rasmi na kuwa hifadhi ya taifa.
Mbuga hii ipo Mikoa ya Pwani na Tanga, kwa upande wa Kaskazini ipo   Wilayani Pangani , Bagamoyo (kaskazini) na Zanzibar.
Kutoka Jiji la Tanga kuna umbali wa kilometa 75 ambapo utapata fursa ya   kuvuka mto Pangani kwa feri huku ukiangalia madhari nzuri ya mji wa Pangani. Pia kuna usafiri wa ndege ambao unaweza kuandaliwa kwenda kiwanja kidogo cha Mkwaja au Saadani.
Tofauti na hifadhi nyingine, mbuga ya Saadani inahifadhi mali kale na wanyama wengine wa majini. Wageni mbalimbali wa ndani na nje ya nchi hutembelea eneo hili ili kujionea maliasili zilizopo sambamba na mandhari nzuri ya hifadhi yenyewe.
Hifadhi hii  ni hifadhi pekee ya wanyama nchini Tanzania inayopakana na Bahari (bahari  ya Hindi) ina fukwe nzuri, jambo linaloifanya iwe ya kuvutia kwa vile ni rahisi  kuona wanyama wakivinjari katika fukwe za bahari.
 Mbali na upatikanaji wa  wanyama kama Parahala hifadhi ina wanyama wa aina nyingi wa baharini na nchi kavu wakiwemo kasa wa kijani, nyangumi wenye nundu na pomboo.
Hifadhi hii inapokea watalii wa ndani na  kutoka nje ya nchi. Nyumba za wageni za TANAPA na vibanda vinapatikana katika kijiji cha Saadani na Makao makuu ya Hifadhi , Mkwaja Wilayani Pangani japo pia kuna maeneo mengi ya kupiga mahema .
Vile vile  Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imewezesha kuwepo kwa hoteli nzuri za kitalii ikiwemo hoteli iliyobeba jina la mbuga ya Saadani inayojulikana kwa jina la “Saadani park hotel”zenye huduma na mazingira   mazuri.
Saadani park Hotel


Written by

1 comment:

  1. Mimi ni mtanzania naitaji kutembelea hifadhi hii je utaratibu upoje kwa ujumla mpaka malazi

    ReplyDelete