HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TANGA YATOA HUDUMA YA UPASUAJI BURE


Hospitali ya Bombo kwa kushirikiana na Madaktari wa Shirika la Interplast la Ujerumani imeanza kutoa huduma ya bure  ya upasuaji wa kurekebisha maumbile kama kupasuka midomo ( cleft lips) kupasuka kaakaa (cleft palate) Uvimbe ( turmors) na Makovu sugu ambayo itakuwepo kwa muda wa siku 10.
Huduma ya upasuaji imeanza kwa uchunguzi wa wagonjwa wenye matatizo hayo kisha kupangiwa tarehe ambapo upasaji wa kwanza umeanza leo tarehe 16/07/2013.
Kwa mujibu wa mratibu wa zoezi hilo la upasuaji Dr Wallace Karata, ushirikiano wa upande hizi mbili katika kunusuru maisha ya Watanzania ulianza  mwaka 2011 ambapo hospitali iliona umuhimu wa kuwasaidia wananchi hasa wale wasio na uwezo wa kulipia upasuaji na matibabu. Jumla ya operation 80 zilifanyika mwaka jana na mwaka huu zaidi ya wagonjwa 50 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji kwa matatizo mabalimbali.
Aidha , uandikishwaji wa wagonjwa wenye matatizo mbalimbali ulianza tarehe 17/6-
10/7/2013 kwa gharama ya shillingi za kitanzania elfu tano ( 5000). Jumla ya  watu wazima 65 na watoto 17 wamejitokeza kufanyiwa uchunguzi wa awali kwa ajili ya upasuaji.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi ambao wametokea pande mbalimbali za nchi  ikiwemo Dar es salaam, wameishukuru Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga,  uongozi wake na shirika la Interplast la Ujerumani kwa huduma hiyo muhimu.

Mtoto Sylvesta Bulaji mwenye umri wa miaka 12 kutoka maeneo ya Mabawa Mkoani Tanga akifanyiwa Uchunguzi  katika Hospitali ya Bombo ili kufanyiwa upasuaji wa mdomo uliopasuka kwa ndani. Miaka 10 iliyopita alifanyiwa upasuaji wa mdomo wa nje uliokuwa umepasuka.

Mtoto Aaliya Maeda mwenye umri wa miaka 2 ½ kutoka Dar es salaam akifanyiwa uchunguzi wa awali wa mkono wake ulioungua vibaya na kusababisha vidole kujikunja kwa ajili ya Upasuaji.

Baadhi ya wagonjwa na ndugu zao waliofika katika Hospitali ya Bombo  kwa ajili ya uchunguzi wa awali


Written by

0 comments: