Tangazo Ukosefu Wa Muda Wa Maji Jijini Tanga


TANGAZO
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (TANGA UWASA) inawatangazia wakazi wa jiji la Tanga kuwa kutakuwa na ukosefu wa maji siku ya Alhamisi ya Tarehe 16/4/2015. Hii inatokana na TANESCO kufanya ukarabati wa nguzo katika maeneo ya mitambo ya maji Pande.

Wananchi mnashauriwa kuhifadhi maji ya kutosha. Huduma inatarajiwa kurejea kama kawaida siku ya Ijumaa tarehe 17/4/2015.

Mamlaka inaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza.


Imetolewa na ofisi ya uhusiano
Tanga uwasa
14/04/2015


Written by

0 comments: