Utepe Mweupe Wakutana Na Waandishi Wa Habari Mkoani Tanga

Bi Rose Mlay, Mratibu wa Muungano wa Utepe Mweupe akitoa mada . Kulia ni Bw. Kenneth Simbaya , Mmoja wa wakufunzi kwenye warsha.


“Mama akiwa salama Taifa liko salama, Mama anapokufa na Taifa linakufa” Hayo ni baadhi ya maneno ambayo waliaswa waandishi wa habari kwenye warsha ya Waandishi wa habari iliyoandaliwa na Muungano wa Utepe Mweupe iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa  Kituo cha Walemavu ( YDCP)

Waandishi  wa Habari kutoka vyombo vya Habari Mkoani Tanga walipata wasaa wa  kuongeza uelewa wa masuala ya Vifo vya Mama na Mtoto. Akizungumza kwa hisia kali, Bi Rose Mlay  ambaye ni Mratibu wa Muungano wa Utepe Mweupe aliwaomba waandishi wa habari kuungana na makundi mengine katika jamii kupaza sauti  kwa niaba ya akina mama ili kupunguza vifo vya mama na mtoto.

“Sababu za vifo vya mama na mtoto hazichagui zinaweza kutokea kwa mama yeyote awe tajiri ama maskini. Mama anahitaji kituo cha afya kilichokaribu na chenye huduma nzuri , vifaa na wataalamu. Jamani Tuwajibike ili mama aishi”

Naye Bw. Kenneth Simbaya , mmoja wa wakufunzi kwenye warsha hiyo alitoa wito kwa waandishi  wa habari kuona umuhimu wa kuandika makala na habari za vifo vya akina mama na watoto ili jamii husika na serikali ilichukulie suala hilo kwa uzito mkubwa.

Warsha ya waandishi wa habari iliyoamdaliwa na Muungano wa Utepe Mweupe ni maandalizi ya maadhimisho ya siku ya Utepe Mweupe yenye kauli mbiu “Wajibika  Mama Aishi”yatakayofanyika kitaifa Machi 15 katika Mkoa wa Tanga.

 Bw. Hassan Hashim, Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanga  ambaye pia ni Mwakilishi wa Channel Ten akichangia mada wakati wa Warsha
Bw.  John Semkande, mwakilishi kutoka Pangani Fm akitoa ushuhuda ni kwa jinsi gani amekuwa akitimiza wajibu wake ili kuhakikisha anaokoa maisha ya mama na mtoto 



Written by

0 comments: