Wakuu Wapya Wa Wilaya Mkoani Tanga Waapishwa Leo

Mhe. Magalula Said Magalula akimwapisha Mhe. Husna Rajab Msangi kuwa  Mkuu wa Wilaya ya Handeni .


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Magalula Said Magalula amewaapishwa leo Wakuu Wapya wa Wilaya ambao ni Mhe. Husna Rajab Msangi, Mkuu wa Wilaya ya Handeni na Mhe. Mariam M. Juma , Mkuu wa Wilaya ya Lushoto wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga .

Mhe. Magalula ameonya tabia ya umangimeza na kuwaasa Wakuu hao wapya kuwa njia pekee ya kumwahakikishia Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa hajakosea kuwateua ni kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii.

Aidha kwa upande wao, Wakuu hao wameomba ushirikiano kutoka kwa viongozi wa Wilaya wanakotoka na Mkoa ili waweze kutekeleza majukumu yao vizuri.

               Mhe Magalula Said Magalula akimwapisha Mhe. Mariam M. Juma kuwa  Mkuu wa Wilaya ya Lushoto .
Baadhi  ya waalikwa wakati wa kiapo

Picha ya pamoja ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Katibu Tawala wa Mkoa Bw. Mohamed Chima ( wa kwanza kushoto kwa waliokaa), wakuu wa Wilaya Wapya , Viongozi Maalumu na  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wilaya




Written by

0 comments: