Jikumbushe Wiki Ya Utepe Mweupe Iliyofanyika Kitaifa Mkoani Tanga

Mkoa wa Tanga umekuwa mwenyeji wa maadhimisho ya Kitaifa ya Utepe Mweupe wa Uzazi salama  yaliyofanyika Machi 15 mwaka huu. Wiki ya Utepe mweupe ilianza tarehe 10 ambapo iliambatana na shughuli mbalimbali zilizolenga kuhakikisha vifo vya mama na mtoto vinavyozuilika vinatokomezwa.

Katika Kupata sauti za Wananchi, Wakazi wa Wilaya tano za Mkoa wa Tanga ambazo ni Kilindi, Handeni, Korogwe, Muheza na Jiji la Tanga walipata fursa ya kutoa maoni yao wakiwawakilisha Watanzania  jinsi gani huduma za afya ziboreshwe  kwa lengo la kupunguza vifo vya mama na mtoto.
Uhamasishaji wa wananchi ulifanyika kupitia vyombo mbalimbali ya habari. Pichani Bi. Agness Mbwana ambaye ni Mratibu wa Utepe Mweupe Mkoa wa Tanga akizungumza  na wananchi juu ya ushiriki wao katika maadhimisho hayo kupitia radio ya Breeze Fm iliyoko Tanga 
Dr Herriet Mwakilishi kutokaChama cha madaktari Wanawake Tanzania  ( MEWATA )  akifafanua kuhusu dalili za awali za ugonjwa wa saratani ya matiti  na huduma za upimaji wakati wa wiki ya  maadhimisho ya Utepe Mweupe Mkoani kupitia radio ya Breeze Fm
 Vikao vya maandalizi ya Utepe Mweupe viliendelea katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga ili kufanikisha zoezi  la maadhimisho kitaifa. Wa pili kulia ni Mganga Mkuu wa mkoa wa Tanga Dr Asha Mahita akifafanua jambo wakati wa kikao
Baadhi ya wajumbe wa vikao vya maandalizi
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Magalula Said Magalula akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini  kwake siku mbili kabla ya Kilele cha Maadhimsho  ili kuutaarifu umma kuwa Mkoa ulijiandaa vyema na maandalizi yalikamilika tayari kwa maadhimisho ya siku ya Utepe Mweupe kitaifa Mkoani Tanga
Baadhi ya waandishi wakati wa mkutano
Zoezi la Upimaji wa dalili za awali ya saratani ya matiti liliiendelea . Pichani akinamama wakisubiri kumwona mtalaamu


Written by

0 comments: