Bodi Ya Barabara Mkoa wa Tanga Yaonya Uharibifu Wa Barabara


Wajumbe wa Bodi ya Barabara Mkoa wa Tanga  wamesikitiswa na baadhi ya tabia za Wakazi wa Tanga ambao kwa makusudi kabisa wamekuwa wakifanya uharibifu katika barabara hasa zile zenye lami. Hayo yamebainika katika kikao cha pili  cha bodi ya barabara kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mku wa Tanga siku ya alhamisi ya Machi 2015 kuanzia saa tatu asubuhi.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Tanga, magalula Said Magalula amesema lengo la kikao cha bodi ya barabaraa ni wadau kupata habari sahihi ya uboreshaji wa barabara katika kupunguza umaskini na kuleta maendeleo kwa wananchi.

“ Tukiweka maazimio mazuri yanayotekelezeka  barabara zetu zinaweza kuwa katika mazingira mazuri na kuhudumia ipasavyo “alisisitiza Magalula

Pia Mhe. Magalula alielekeza Wakurugenzi wa Halmashauri za tanga kuhakikisha wanatoa  elimu kwa wananchi juu ya kutumia vivuko vilivyowekwa barabarani rasmi kwa ajili ya kuvusha mifugo.


Kikao kiliazimia  kuhakikisha uboreshaji katika kudhibiti uzito na mifugo kutembea barabarani.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga , Mhe Magalula Said Magalula akifungua rasmi kikao cha Bodi ya barabara
Meneja wa TANROADS Mhandisi Alfred Ndumbaro Akitoa taarifa ya hali ya barabara katika Mkoa wa Tanga
 Mbunge wa jimbo la  Tanga Mhe Omari Nundu akichangia mada wakati wa Kikao
Baadhi ya wajumbe wa bodi ya Barabara na waalikwa




Written by

0 comments: