Kamati Ya Bunge Ya Kilimo, Maji Na Mifugo Yaonya Uharibifu Wa Mazingira katika Vyanzo vya Maji


 Uchimbaji wa madini katika chanzo cha maji cha mto Zigi uliopo eneo la Amani Wilaya ya Muheza umeendelea kuleta madhara  makubwa kwa kusababisha kupungua kwa maji ambayo awali yamekuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa Tanga.

Hayo yamebainika wakati wa ziara ya siku moja ya Kamati  ndogo ya Bunge ya Kilimo, Maji na Mifugo ilipotembelea katika eneo hilo  mwanzoni mwa wiki  ikiwa ni sehemu ya ukaguzi wa miradi ya maji katika Mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara

Akizungumza mara baada ya kusomewa taarifa ya maendeleo ya chanzo cha maji ya mto Zigi, Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Bunge Mhe. Moshi Selemani Kakoso ameutahadharisha umma kuwa muda uliobaki si wa kulalamikia madhara bali  kila mwananchi ana jukumu la  kuchukua hatua katika utunzaji wa mazingira.

“Wafichueni waharifu wa mazingira kwani waharibifu sio wageni bali ni miongoni mwa wakazi wa eneo husika” alisisitiza Mhe. Kakoso

Vile vile wito umetolewa kwa Uongozi wa Mamlaka ya Maji Tanga kuhakikisha kuwa wanabuni miradi ya maendeleo ambayo ni endelevu ili kuwawezesha wananchi kuachana na uchimbaji wa madini katika eneo la chanzo cha maji.

Wakijibu hoja ya Miradi ya mendeleo, Mamlaka ya maji Tanga imesema tayari ipo miradi mbalimbali ambayo inaendeshwa na Mamlaka hiyo na kiasi cha shilingi millioni 100 zimeshatengwa kwa mwaka 2014/15 kwa ajili ya kuboresha maisha ya wakazi ambao wanaishi eneo karibu na chanzo cha maji cha mti Zigi.

Nao wananchi wakizungumza wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha  Sangarawe ambacho kipo karibu na hifadhi ya taifa ya Amani, wameiomba serikali kuona uwezekano wa kuboresha  barabara ili kusaidia usafirishaji wa mazao kwenda muheza mjini.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya Muheza amewakumbusha wananchi kuwa tayari serikali imeshaanza mchakato wa kuendeleza barabara hiyo na kwa sasa iko katika kiwango cha changalawe na jitihada zinafanyika ili barabara hiyo iweze kuwekwa katika kiwango cha lami katika siku za usoni.
Katibu Tawala Msaidizi  kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tanga Eng. Ephraim Minde akifafanua jambo mara baada ya Kamati ya Bunge na wawakilishi kutoka Wizara ya Kilimo kuwasili ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Muheza 

 Mjumbe wa Kamati ya Bunge Mhe Subira K. Mgalu  ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Muheza akitoa ufafanuzi na kuonyesha uharibifu unaoendelea katika eneo la Chanzo cha maji cha mto Zigi eneo la Amani Wilaya ya muheza mara baada ya kutembelea eneo la Sangarawe. Kulia kwake ni mjumbe wa Kamati  Vrajlal Son.

 Taswira ya sasa ya baadhi ya   eneo la Sangarawe  baada ya uchimbaji wa madini usio rasmi unaofanywa na vijana wa eneo hilo




 Bw. Shaban Hamis Mzava- Meneja wa Mamlaka ya Maji Wilaya ya Muheza akisoma taarifa ya mradi wa Maji  Kijiji cha Ubembe Wilaya ya Muheza mara baada ya Kamati ya Bunge ya kilimo, Maji na Mifugo kutembelea Mradi huo.

 Kamati ikitembelea mradi huo
Mradi wa maji Kijiji cha  Ubembe Wilaya ya Muheza


Written by

0 comments: