Serikali Yasema Zoezi La Kupigia Kura Katiba inayopendekezwa Liko Pale Pale

Serikali imewahikikishia watanzania kuwa zoezi la uandikishwaji wa wapiga kura katika daftari la kudumu kwa mfumo wa kieletroniki BVR litafanyika kwa ufanisi na ndani ya wakati uliopangwa.

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda Bungeni leo wakati akijibu  swali la kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni Mhe. Freeman Mbowe kuhusu uhakika wa zoezi hilo na pia ameuhakikishia umma kuwa vifaa vinavyotarajiwa  kuletwa vina ubora mara ya mbili ya vilivyoletwa mwanzo kwa ajili ya zoezi la majaribio hilo.

Mhe. Pinda amewataka wananchi wasiwe na wasiwasi bali wajiandaa vyema kwa   kuwa zoezi la upigaji kura kwa ajili ya katiba mpya litafanyika katika tarehe iliyopangwa .
  
Vile vile Mhe. Pinda amesisitiza kuwa  endapo tume itaona kuwa zoezi hilo haliwezekani kwa sababu yoyote ile, itatoa taarifa serikalini na serikali iko tayari kubadili maamuzi.
  
Zoezi la kupiga kura ya maoni linatarajiwa kufanyika April 30 mwaka huu .




Written by

0 comments: