Mahakama Tanga Yazindua Bodi Mpya Ya Parole


 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Magalula Said Magalula amewataka wajumbe wa Bodi ya Paroli Mkoa  kutenda kazi kwa kufuata kanuni na taratibu zilizowekwa ili kutenda haki na kuepuka ushawishi wa namna yeyote katika kupokea na kuomba rushwa.

Hayo yamesemwa mapema siku ya alhamisi ya machi 12 mwaka huu wakati wa uzindua rasmi Bodi ya Parole Mkoa tukio lililofanyika katika ofisi za Magereza Mkoa.

 Lengo la Bodi hii ni  kuwajadili  wafungwa wenye sifa  za kuweza kuachiliwa huru baada ya kutimiza vigezo ambavyo vimeainishwa kwenye  sheria namba 25  ya Paroli ya mwaka 1994 na kufanyiwa mabadiliko mwaka 2002.

Sheria husika imeweza kuanisha ni aina gani ya makosa ambayo mfungwa anaweza kupata fursa ya kuingia kwenye mpango wa Paroli . Pamoja na makosa hayo mfungwa hawezi kuingizwa kwenye utaratibu wa Paroli endapo amepatikana na kosa la unyanyanyi wa siraha, madawa ya kulevya, kulawiti, kubaka na mauaji ya kukusudia.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa sheria ya parole tangu utekelezaji wake mwaka 2003, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga Kamishina Agustino Mboje amesema tayari wafungwa 331 wameshaachiliwa huru kwa utaratibu wa parole, wafungwa 305 wamemaliza vifungo vyao salama na wafungwa 26 bado wanaendelea na vifungo vyao kwa utaratibu huu.

Licha ya kuwepo na mpango huu wa kupunguza msongamano wa wafungwa gerezani lakini bado wafungwa wengi wameshindwa kunufaika na utaratibu wa Paroli kutokana na kutotimiza masharti ya parole.

Sababu kubwa ni ukosefu wa nakala za hukumu kwa wakati na ukosefu wa elimu ya kutosha  kwa wanajamii kuhusu sheria hii na hivyo kupelekea maafisa wa Paroli  kuwa na ugumu wa kupata taarifa muhimu zinazowahusu wafungwa wananotarajiwa kunufaika na mpango huu.

 Maafisa wa Magereza wakimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Magalula Said Magalula
Mkuu wa Mkoa wa Tanga akisaini kitabu cha wageni
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga Kam. Augostino Mboje akitoa taarifa ya utekelezaji wa sheria ya Parole katika Mkoa wa Tanga
Baadhi ya wajumbe na Maafisa wa magereza wakati wa uzinduzi



Written by

0 comments: